Verse 1
Aleluya tumwabudu Yesu Kristu
Yu hai mzima katika ekaristi
Aleluya aleluya aleluya
Verse 2
Sakramenti kuu hii ya mapendo,
Ulimojiweka kwa ajili ya watu,
Nasi twakupa yetu leo mapendo.
Verse 3
Ni sadaka ya msalaba twaijua,
Kafufuka kisha kapaa kwa Baba,
Yuko nasi katika hii Ekaristi.
Verse 4
Ni chakula chetu bora na kwa roho,
Ni Mwanakondoo yule wa pasaka,
Atulisha, atushibisha daima.
Verse 5
Njoni wote tumwabudu Yesu Kristu,
Nyoyo zetu, nyimbo zetu tumtolee,
Sifa zetu, shangwe zetu tumpatie.
Verse 6
Mwili wako uwe asili ya heri,
Utakase nyoyo zetu kwa damuyo,
Zifike mbinguni daima milele.n
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.