Angalia Jinsi Mkulima
{Angalia jinsi mkulima anavyofurahi-ya, kuyachuna matunda (yale) yalivyo vizuri katika bustani yake}*2
Na pia kuyatupa yale mabovu mbali
Na kuyaacha yaliyo mabichi ili yapate kuiva vizurinili aweze kuyachambua tena
Vivyo hivyo Mungu hufurahia kuwaita kwake wale walioa safi
Na kuwapa nafasi ya kutubu wale wenye dhambi
Ni wajibu kwangu mimi na wewe, kutubu kwani hakuna ajuaye siku
Wala saa ambayo Mungu Baba atamwita kwake
Ewe ndugu yangu unafikiria nini kuingia katika jubilei
Ya miaka elfu mbili ukiwa na mzigo wa dhambi
Yafaa nini mtu kupata raha zote za dunia ambazo ni za muda
Na kutupwa katika moto ule wa milele yote
Mimi na wewe tutumie nafasi hii tuliyopewa tutubu dhambi zetu
Mtu asijeijutia siku atakayoitwa
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.