Asante Kwa Wema
Bwana alinitendea mambo makuu
Nilipoita jina lake aliniitikia
Alinitegemeza katika taabu zangu
{ Asante- kwa wema wako
Asante-kwa ukarimu
Asante kwa pendo lako nashukuru } * 2
Bwana ameniponya na magonjwa mengi
Pia amenikinga na ajali mbaya sana
Amenitoa katika mitego ya shetani
Nimetafakari upendo wake Bwana
Kujivika ubinadamu na kufa msalabani
Ili nikombolewe utumwani wa shetani
Ni mara nyingi sana nimetenda dhambi
Lakini Bwana Yesu hakunihukumu kwa dhambi
Hakuna kama Bwana yeye ni Mungu pekee
Wema wake Mungu wangu hauna mwisho
Ameniandalia makao baada ya kifo
Masharti yake niwe nimetii amri za Mungu
Enyi ndugu zangu mlio katika Kristu
Unganeni pamoja nami kumshukuru Mungu
Ni mema mengi sana yeye ametujalia
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.