SectionsThanksgivingAsante Kwa Wema

Asante Kwa Wema

Ordinary Time,MarianThanksgiving
Verse 1

Bwana alinitendea mambo makuu

Nilipoita jina lake aliniitikia

Alinitegemeza katika taabu zangu

Chorus

{ Asante- kwa wema wako

Asante-kwa ukarimu

Asante kwa pendo lako nashukuru } * 2

Verse 3

Bwana ameniponya na magonjwa mengi

Pia amenikinga na ajali mbaya sana

Amenitoa katika mitego ya shetani

Verse 4

Nimetafakari upendo wake Bwana

Kujivika ubinadamu na kufa msalabani

Ili nikombolewe utumwani wa shetani

Verse 5

Ni mara nyingi sana nimetenda dhambi

Lakini Bwana Yesu hakunihukumu kwa dhambi

Hakuna kama Bwana yeye ni Mungu pekee

Verse 6

Wema wake Mungu wangu hauna mwisho

Ameniandalia makao baada ya kifo

Masharti yake niwe nimetii amri za Mungu

Verse 7

Enyi ndugu zangu mlio katika Kristu

Unganeni pamoja nami kumshukuru Mungu

Ni mema mengi sana yeye ametujalia

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.