Chorus
{Bwana aliniambia, ndiwe mwanangu,nmimi leo nimekuzaa leo, nimekuzaa leo }* 2
Verse 2
Wafalme wa dunia wanajipanga na wakuu,
Wanafanya shauri pamoja juu ya Masiha wake.
Verse 3
Yeye anayeketi huko mbinguni anacheka,
Naye Bwana anawafanyia dhihaka hao wafalme.
Verse 4
Bwana aliniambia ndiwe mwana wangu,
Mimi nimekuzaa leo, nimekuzaa leo.
Verse 5
Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu,
Kama mwanzo, sasa na siku zote milele amina.
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.