Verse 1
Bwana ni mchunga, sitahitaji.
Majani mabichi, malisho yangu.
Ananinywesha maji matulivu
Atanirudisha nikipotea
Verse 2
Nipitapo bondeni mwa mauti,
U mlinzi wangu, sitaogopa.
Fimbo lako latosha kunilinda.
Ukinifariji sina hasara.
Verse 3
Kati ya mateso meza waandaa
Na kikombe changu kinafurika
Umenipaka kichwani mafuta.
Nitaulizaje zaidi kwako.
Verse 4
Wema na fadhili vinifuate
Siku zangu zote, hata milele.
Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana.
Katika ufalme wa pendo lake.n
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.