SectionsExitBwana Ni Mchungaji

Bwana Ni Mchungaji

Ordinary TimeExit
Verse 1

Bwana ni mchunga, sitahitaji.

Majani mabichi, malisho yangu.

Ananinywesha maji matulivu

Atanirudisha nikipotea

Verse 2

Nipitapo bondeni mwa mauti,

U mlinzi wangu, sitaogopa.

Fimbo lako latosha kunilinda.

Ukinifariji sina hasara.

Verse 3

Kati ya mateso meza waandaa

Na kikombe changu kinafurika

Umenipaka kichwani mafuta.

Nitaulizaje zaidi kwako.

Verse 4

Wema na fadhili vinifuate

Siku zangu zote, hata milele.

Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana.

Katika ufalme wa pendo lake.n

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.