SectionsExitChenga Ya Mwili

Chenga Ya Mwili

Baptism,BaptismExit
Chorus

Nimempiga shetani chenga ya mwili

Kuisalimisha roho yangu kuisalimisha roho

Nimempokea Yesu moyoni mwangu

Nipate uzima wa milele ili niishi milele

Verse 2

Tazama nimebatizwa kwa nafsi tatu

Baba mwana naye Roho Mtakatifu

Nimempokea Kristu moyoni mwangu

Kwa mwili na damu yake nimeshibishwa

Verse 3

Nimempokea Roho Mtakatifu

Amenijaza mapaji mapaji saba

Nimeikiri imani, imani yangu

Nimemkana shetani na mambo yake.

Verse 4

Nikikumbuka kiapo cha ubatizo

Najionea fahari ya ukristu wangu

Nikikumbuka ungamo la dhambi zangu

Ninaukiri upendo wa Yesu Kristu.

Verse 5

Nimeshamweka kando, shetani mwovu

Aliye mpotoshaji wa mambo mema

Alishaniweka kwenye, imaya yake

Alinidanganya sana na mambo yaken

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.