Chorus
{ Ee nafsi yangu mhimidi Bwana, wewe Bwana Mungu wangu,numejifanya mkuu sana, umejivika heshima na adhama } * 2
Verse 2
Umejivika nuru kama vazi, umezitandaza mbingu kama pazia
Na kuziweka nguzo za horofa, nguzo za horofa zake majini
Verse 3
Huwafanya malaika zake, huwafanya kuwa pepo
Na watumishi watumishi wake, huwafanya kuwa moto wa miali
Verse 4
Ee Bwana jinsi yalivyo mengi, yalivyo mengi matendo yako
Kwa heshima umefanya vyote, dunia imejaa mali yako
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.