Verse 1
Ee ndugu peleka talanta yako kwa Bwana
Kwani Mungu alikupatia kwa kiasi chako
Nawe mrudishie Bwana kama wale watumishi
Kama wale waliopewa talanta mbili na tano
Verse 2
Kumbuka waliopewa talanta mbili na tano
Walileta mbili na tano faida
Bwana wao akawasifu kwa uaminifu wao
Akawapokelea nao akawakweza
Verse 3
Kumbuka aliwapatia tunzo la ufalme
Kwa hao waaminifu kwa hayo machache
Nao wakapewa yaliyo makubwa kwa bwana wao
Na sisi tupeleke talanta zetu kwa Bwana
Verse 4
Kumbuka Mungu alivyokupatia kwa wiki nzima
Atataka kufanya hesabu nawe
Ukumbuke kutoa hesabu kama wale wawili
Naye Bwana Mungu wako atakupokelea
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.