SectionsOffertoryEe Ndugu Peleka

Ee Ndugu Peleka

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,MarianOffertory
Verse 1

Ee ndugu peleka talanta yako kwa Bwana

Kwani Mungu alikupatia kwa kiasi chako

Nawe mrudishie Bwana kama wale watumishi

Kama wale waliopewa talanta mbili na tano

Verse 2

Kumbuka waliopewa talanta mbili na tano

Walileta mbili na tano faida

Bwana wao akawasifu kwa uaminifu wao

Akawapokelea nao akawakweza

Verse 3

Kumbuka aliwapatia tunzo la ufalme

Kwa hao waaminifu kwa hayo machache

Nao wakapewa yaliyo makubwa kwa bwana wao

Na sisi tupeleke talanta zetu kwa Bwana

Verse 4

Kumbuka Mungu alivyokupatia kwa wiki nzima

Atataka kufanya hesabu nawe

Ukumbuke kutoa hesabu kama wale wawili

Naye Bwana Mungu wako atakupokelea

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.