SectionsExitHazina Ya Mvivu

Hazina Ya Mvivu

Ordinary Time,Ordinary Time,MarianExit
Chorus

Hazina ya Mvivu ni maneno ya uongo (na tena)

Furaha ya mvivu ni kugombanisha watu

Verse 2

Hawezi kulala kapata usingizi usiku

Usiku mzima hukodoa macho akiwaza

Kukipambazuka aende kwa nani kupiga umbeya

Verse 3

Asubuhi mapema huamka na kuvaa nguo

Hajafagia nyumba huyo huyo kwa jirani kaenda

Hodi jirani jirani naye karibu tupo unasemaje

Atapiga umbea hapo hadi chakula cha mchana ale

Verse 4

Akipitapita mitaani huwa amependeza

Salamu kwa watu utasema huyu ni mtu mwema

Kumbe ni muovu asiye kuwa na aibu kwa watu

Verse 5

Wenzake wanaamka mapema na kwenda kazini

Yeye akiamka huyo huyo safari kwenye pombe

Akishafika huko tazama anavyolewa wala hawazi

Familia yake itakula nini mchana na usiku

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.