Chorus
Hazina ya Mvivu ni maneno ya uongo (na tena)
Furaha ya mvivu ni kugombanisha watu
Verse 2
Hawezi kulala kapata usingizi usiku
Usiku mzima hukodoa macho akiwaza
Kukipambazuka aende kwa nani kupiga umbeya
Verse 3
Asubuhi mapema huamka na kuvaa nguo
Hajafagia nyumba huyo huyo kwa jirani kaenda
Hodi jirani jirani naye karibu tupo unasemaje
Atapiga umbea hapo hadi chakula cha mchana ale
Verse 4
Akipitapita mitaani huwa amependeza
Salamu kwa watu utasema huyu ni mtu mwema
Kumbe ni muovu asiye kuwa na aibu kwa watu
Verse 5
Wenzake wanaamka mapema na kwenda kazini
Yeye akiamka huyo huyo safari kwenye pombe
Akishafika huko tazama anavyolewa wala hawazi
Familia yake itakula nini mchana na usiku
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.