Chorus
{ Hiki ndicho chakula bora kwa wanyofu wa moyo
Wote wenye mioyo safi Bwana awaalika } *2n{ /s/ a/t/b/
Haya njoni wote mezani kwa chakula bora cha uzima
Haya njoni wote mezani kwa chakula bora
Haya njoni kwa chakula bora, cha uzima
Wana heri wale wote, wanaokipokea } *2
Verse 2
Kwa upendo Bwana Yesu amejitoa kama chakula
Bwana akajitoa, apate kuziokoa roho zetu.
Verse 3
Njooni wote wenye kiu ya kupokea wokovu wake
Njooni maskini, njoni viwete vipofu na wagonjwa
Verse 4
Tule tunywe siku zote kwa ukombozi wa roho zetu
Haya njoni wote, mezani kwa Bwana kwa chakula bora
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.