Chorus
Hili ni fumbo la imani, Kristu alikufa
Kristu alifufuka, Kristu atarudi tena
Verse 2
Bwana Yesu alhamisi kuu kajitolea,
Mwili na damu yake ziwe kiburudisho
Akatuamuru tukipenda kumkumbuka,
Mwili na damu ni ishara ya penzi lake
Verse 3
Alaye mwili na kunywa damu asema Bwana
Aishi ndani yangu na mimi ndani yake
Yeye ni rafiki yangu na nitamfufua,
Nitaandamana naye safarini mwake
Verse 4
Alaye mwili wa Yesu na kuinywa damu,
Bila stahili ana hukumu ya milele
Tujitakase kabla ya kula karamuyo,
Kitubio ni sakramenti ya mapatano
Verse 5
Ee Yesu nipe neema ya kukupokea,
Unipe nguvu ya kuweza kujitakasa
Unijalie kukupenda na moyo wote,
Mwishowe nishiriki karamu ya Mbinguni
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.