SectionsEucharistHili Ni Fumbo La Imani

Hili Ni Fumbo La Imani

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeEucharist
Chorus

Hili ni fumbo la imani, Kristu alikufa

Kristu alifufuka, Kristu atarudi tena

Verse 2

Bwana Yesu alhamisi kuu kajitolea,

Mwili na damu yake ziwe kiburudisho

Akatuamuru tukipenda kumkumbuka,

Mwili na damu ni ishara ya penzi lake

Verse 3

Alaye mwili na kunywa damu asema Bwana

Aishi ndani yangu na mimi ndani yake

Yeye ni rafiki yangu na nitamfufua,

Nitaandamana naye safarini mwake

Verse 4

Alaye mwili wa Yesu na kuinywa damu,

Bila stahili ana hukumu ya milele

Tujitakase kabla ya kula karamuyo,

Kitubio ni sakramenti ya mapatano

Verse 5

Ee Yesu nipe neema ya kukupokea,

Unipe nguvu ya kuweza kujitakasa

Unijalie kukupenda na moyo wote,

Mwishowe nishiriki karamu ya Mbinguni

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.