Hima Hima Najongea

Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimePresentation of Gifts
Chorus

{ Hima hima leo, najongea kwako Bwana,

Ninakuja kwako kwa unyenyekevu wangu,

Nakuletea matunda ya jasho langu,

Pokea Baba nami unipe Baraka } *2

Verse 2

[ t ] Kwa ukarimu nimejitolea mimi mwenyewe,

Polepole nasonga mbele nifike kwako,n[ w ] Nikukabidhi nilicho nacho, hiki kidogo Baba pokea.

Verse 3

Mapato yangu ni duni sana, we wanijua,

Sina kitu kizuri cha kukuletea wewe,

Nakukabidhi maisha yangu, uzima wangu Baba pokea.

Verse 4

Mungu wangu ninakuja kwako nikushukuru,

Umenilinda siku zote asante sana,

Mavuno yangu nakupa wewe, na fedha zangu Baba pokea.

Verse 5

Wiki nzima umenijalia uhai bure,

Umenikinga na matatizo unanipenda,

Mkate huu nakutolea, divai hii Baba pokea.

Verse 6

Baraka zako ninazipokea siku kwa siku

Mungu Baba nionyeshe Mbingu nifanye kazi,

Mifugo yangu nakuletea, furaha yangu Baba pokea.

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.