SectionsBible ProcessionHubirini Kwa Sauti (Ii)

Hubirini Kwa Sauti (Ii)

Ordinary TimeBible Procession
Chorus

Hubirini kwa sauti ya kuimba, tangazeni haya

Hubirini kwa sauti ya kinanda, tangazeni haya

Yatamkeni, tamkeni hadi mwisho wa dunia

Semeni Bwana amelikomboa taifa lake

Verse 2

Mwimbieni Bwana wimbo ule mpya,

Mwimbieni Bwana enyi mataifa

Mwimbieni Bwana kwa sauti ya shangwe,

Mwimbieni Bwana libarikini jina lake

Verse 3

Tangazeni wokovu siku kwa siku,

Hubirini habari za utukufu

Yahubirini mataifa sifa zake,

Na watu wote habari za ukuu wake

Verse 4

Mpeni Bwana utukufu na nguvu,

Mpeni Bwana enyi wana wa Mungu

Pelekeni habari zake pande zote,

Mpeni Bwana utukufu wa jina laken

Verse 5

Mwabuduni Bwana kwa utakatifu,ntetemekeni mbeleze nchi yote

Semeni kwamba Bwana ametamalaki,

Atawahukumu watu wake kwa adili

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.