Ikulu Ya Mbinguni
Ordinary Time,Ordinary Time,Lent,Resurrection,Ordinary TimeThanksgiving
Chorus
{ Ukimcha Bwana Mungu (katika) maisha yako yote
Hakika utakaribishwa (kwenye) ikulu ya Mbinguni } *2
Verse 2
Tazama Mungu ni hodari (sana) wala hamdharau mtu yeyote
Naye ana uwezo (mwingi) katika kufunza ufahamu mwingi
Verse 3
Hufungua masikio (yako) yasikie maonyo yake mwenyezi
Na kukuagiza (urudi) kwake na kuuacha uovu wako wote
Verse 4
Kama wewe ukisikia (wewe) na kumtumikia atapitisha siku zako
Na mafanikio (mengi) na miaka yenu katika furaha
Verse 5
Na ukithamini zaidi (mali) kuliko roho yako utaangamia
Na kufaa pasipo (maarifa) hautauona uso wa Mungu
Verse 6
Basi jitunze isije (hasira) ikakuvuta ama ukafanya mzaha
Wala usikubali (kamwe) ukuu wa ukombozi ukutawale
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.