SectionsExitKaeni Katika Pendo

Kaeni Katika Pendo

Wedding,Wedding,Ordinary TimeExit
Chorus

Kama vile Baba alivyonipenda mimi

Nami nilivyo wapenda ninyi

Kaeni katika pendo langu

Kaeni - katika pendo (langu) * 2

Kaeni katika pendo langu

Verse 2

Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu

Kama vile mimi nilivyozishika, amri za Baba yangu

Na kukaa katika pendo lake

Verse 3

Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu

Na furaha yenu itimizwe

Verse 4

Amri yangu ndiyo hii, mpendane kama nilivyowapenda

Kama nilivyowapenda ninyi

Verse 5

Hamna aliye na upendo, upendo mwingi kuliko huu

Wa mtu kutoa uhai wake, kwa ajili ya rafiki zake

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.