Chorus
Kama vile Baba alivyonipenda mimi
Nami nilivyo wapenda ninyi
Kaeni katika pendo langu
Kaeni - katika pendo (langu) * 2
Kaeni katika pendo langu
Verse 2
Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu
Kama vile mimi nilivyozishika, amri za Baba yangu
Na kukaa katika pendo lake
Verse 3
Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu
Na furaha yenu itimizwe
Verse 4
Amri yangu ndiyo hii, mpendane kama nilivyowapenda
Kama nilivyowapenda ninyi
Verse 5
Hamna aliye na upendo, upendo mwingi kuliko huu
Wa mtu kutoa uhai wake, kwa ajili ya rafiki zake
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.