Chorus
{Kama vile mwili ni mmoja nao unao viungo vingi
Tena na viungo vyote vya mwili ulonavyo ni vingin(Kweli) Ni mwili mmoja }*2n{Vinafanya kazi zote, kwa pamoja siku zote
Kwani vyote vya maana, na vizuri kwelikweli
Nasi sote Wakristu tushirikiane }*2
Verse 2
Kwa maana katika Roho, sisi sote tulibatizwa
Tulinyweshwa Roho mmoja, basi sote ni mwili mmoja
Verse 3
Kama sisi ni Wayahudi au sisi ni Wayunani
Tukiwa ndani ya Yesu hatuko tofauti kabisa
Verse 4
Miguu, mikono na macho masikio hata mapua
Na viungo vyote vya mwili vinafanya kazi kwa pamoja
Verse 5
Katika kanisa la Bwana sisi sote tuna nafasi
Tutumie nafasi zetu kwa huduma ya kanisa lake
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.