SectionsExitKama Vile Mwili

Kama Vile Mwili

Ordinary Time,Ordinary TimeExit
Chorus

{Kama vile mwili ni mmoja nao unao viungo vingi

Tena na viungo vyote vya mwili ulonavyo ni vingin(Kweli) Ni mwili mmoja }*2n{Vinafanya kazi zote, kwa pamoja siku zote

Kwani vyote vya maana, na vizuri kwelikweli

Nasi sote Wakristu tushirikiane }*2

Verse 2

Kwa maana katika Roho, sisi sote tulibatizwa

Tulinyweshwa Roho mmoja, basi sote ni mwili mmoja

Verse 3

Kama sisi ni Wayahudi au sisi ni Wayunani

Tukiwa ndani ya Yesu hatuko tofauti kabisa

Verse 4

Miguu, mikono na macho masikio hata mapua

Na viungo vyote vya mwili vinafanya kazi kwa pamoja

Verse 5

Katika kanisa la Bwana sisi sote tuna nafasi

Tutumie nafasi zetu kwa huduma ya kanisa lake

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.