Kivumbi
Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Lent,Christmas,Ordinary Time,Resurrection,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Easter,Christmas,Ordinary Time,Ordinary Time,Christmas,Ordinary TimeThanksgiving
Verse 1
Hapo ndipo tulipomfurahia Bwana Mungu wetu
Hirizi na mizimu yote viliposhindwa kusimama
Shetani naye kivumbi kakitimua kakimbia
Chorus
{Hapo ndipo tukasema hebu Mungu aitwe Mungu
Hapo ndipo tukasema yeye apewe sifa
Hapo ndipo tukasema atawale Mungu milele } *2
Verse 3
Tazama Bwana alipounyoosha mkono wake mkuu
Wachawi wote wakakoma, mapepo na yakanyamaza
Waganga na tunguri zao kwa aibu wakaduwaa
Verse 4
Bwana alipoinua mkono hodari kwa wagonjwa
Wakoma wakatakasika viziwi wakasikia
Viwete wakarukaruka kwa furaha wamepona
Verse 5
Jicho la Bwana lilipowaelekea watu waovu
Hasira, chuki na majivuno vyote vikatoweka
Kiburi na maringo yao hapo ndipo vikapotea
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.