Kivumbi

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Lent,Christmas,Ordinary Time,Resurrection,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Easter,Christmas,Ordinary Time,Ordinary Time,Christmas,Ordinary TimeThanksgiving
Verse 1

Hapo ndipo tulipomfurahia Bwana Mungu wetu

Hirizi na mizimu yote viliposhindwa kusimama

Shetani naye kivumbi kakitimua kakimbia

Chorus

{Hapo ndipo tukasema hebu Mungu aitwe Mungu

Hapo ndipo tukasema yeye apewe sifa

Hapo ndipo tukasema atawale Mungu milele } *2

Verse 3

Tazama Bwana alipounyoosha mkono wake mkuu

Wachawi wote wakakoma, mapepo na yakanyamaza

Waganga na tunguri zao kwa aibu wakaduwaa

Verse 4

Bwana alipoinua mkono hodari kwa wagonjwa

Wakoma wakatakasika viziwi wakasikia

Viwete wakarukaruka kwa furaha wamepona

Verse 5

Jicho la Bwana lilipowaelekea watu waovu

Hasira, chuki na majivuno vyote vikatoweka

Kiburi na maringo yao hapo ndipo vikapotea

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.