Kwa jinsi ujionavyo (ndivyo) ndivyo ulivyoumbwa
Tena kwa mfano wake Yesu Kristu Mwokozi wetu
Furaha leo tuimbe shangwe
Tupige ngoma filimbi na vigelegele
Tufurahi tufurahi na Bwana Yesu
Yeye mwenyewe aliona kwa jinsi hii utapendeza
Sasa mbona wewe wamsahau Bwana Mungu wako
Waisahau hata Sabato siku ya kumshukuru Mungu
Tusijiongeze vitu vingine ndugu vya kujipamba
Njoo kwake Bwana Yesu atakupamba upendeze
Ili uweze kufika kwake Mungu kwenye uzima milele
Ni Yesu Kristu peke yake aliye na upendo zaidi
Katuandalia karamu kabla ya mauti yake
Kaibariki kila tuilapo tupate uzima milele
Ulapo bila kustahili ndugu ungoje hukumu yako
Alisema mwenye moyo safi ajongee mezani
Siku ile ya hukumu nitamwita kwenye ufalme Mbingunin
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.