SectionsEntranceKwa Nini Wanipiga

Kwa Nini Wanipiga

Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,LentEntrance
Chorus

{ Kama nimesema vibaya toa ushahidi wa neno baya

Bali kama nimesema vema kwanini wanipiga? } *2

Verse 2

[ s ] Pilato alimhukumu Yesu, ingawa hakuona kosa kwake

Aliwaogopa Wayahudi, na kubembeleza urafiki wa Kaisari

Verse 3

Ndugu yangu tafakari kwa makini, mamlaka ulopewa na wenzio

Unayatumia ipasavyo au waumiza wenzako kama Pilato

Verse 4

Askari usalama wa raia, acheni kuwadhulumu raia,

Na kusingizia watu kesi, mnasababisha uvunjaji wa sheria

Verse 5

Mahakimu na mabingwa wa sheria, haifai kuipotosha sheria,

Maskini wajane na yatima mnawanyang`anya haki zao hukumuni

Verse 6

Waganga wakunga na wauguzi, tibuni bila kudai zawadi,

Watu masikini na yatima wanahangaika vitandani hadi kufa

Verse 7

Wanandoa tunzeni ahadi zenu, kupendana katika shida na raha,

Pia kuwalea wana katika njia impasayo Mkristo

Verse 8

Utoaji wa mimba bila sababu, na kutupa watoto majalalani,

Ni kutoujali utu wa mtu, na kuwahukumu kifo wasio na kosa

Verse 9

Dunia yetu inawaka moto, amani yetu imeshatoweka,

Vita vyatawala kila kona kisa ni tamaa ya mali na madaraka

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.