Litukuzeni Jina
Litukuzeni Jina la Mungu daima milele
Enyi mataifa, mshangilieni Mungu wetu
Kwa kuwa Bwana ni Mtukufu wa kutisha
Yeye ni mfalme mkuu wa dunia yote
Sifuni Bwana kwa shangwe
{Jina la Mungu lihimidiwe daima milelen( litukuzwe litukuzwe litukuzwe litukuzwe litukuzwe litukuzwe)
Enyi mataifa mhimidini
Kwa kuwa fadhili zake (kwetu sisi) zadumu daima milele } *2
Jina lake Bwana litukuzwe sasa hata milele
Viumbe vya Bwana Sifuni Bwana Mungu wetu
Toka mawio hata machweo ya jua
Sifuni jina lake Bwana Mungu wetu
Sifuni Bwana Mwenyezi
Enyi watumishi sifuni Bwana kutoka Mbinguni
Mbingu nanyi maji, lisifuni jina la Bwana
Wafalme wa dunia nanyi watu wote
Wakuu nanyi wakaazi wote wa dunia
Sifuni Bwana Mwenyezi
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.