SectionsEntranceMalaika Kaleta Noeli

Malaika Kaleta Noeli

ChristmasEntrance
Verse 1

Malaika kaleta Noeli ya kwanza,

Kwa wachunga kondoo katika makonde,

Bethlehemu wakawa walinzi wa zamu,

Wakaona usiku ajabu ya nuru

Chorus

{ Noeli, Noeli, Noeli, Noeli,

Yesu yu Mungu na binadamu } *2

Verse 3

Wakaona mbinguni, mwangaza wa nyota,

Ing'aayo kwa mbali na masharikini,

Wakaenda upesi, walivyoambiwa.

Bethlehemu wamwone Mwokozi horini

Verse 4

Mashariki watoka wafalme watatu,

Mamajusi waliotafuta mfalme,

Wafuata hii nyota waliyoiona,

Wasipate kumkosa wanayemtafuta

Verse 5

Kiongozi ni nyota iliyowaleta

Hata mji wa Daudi alimozaliwa

Ikakaa mara moja isiendelee

Pale pale nyumbani alimo Mwokozi

Verse 6

Mamajusi walipoingia nyumbani

Wakapiga magoti kwa heshima kuu

Mara hiyo walipozifungua hazina

Manemane, uvumba, dhahabu, watoa

Verse 7

Basi sisi wakristu na tumsujudie

Tumhimidi Mwokozi, aliyeviumba

Vitu vyote mbinguni duniani na sisi

Na ametufia na kutukomboa

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.