Mambo Ya Yesu
{ Hatutaacha kuyanena mambo ya Yesu
Hatutaacha kuyasimulia matendo yake Kristu } *2n(Sisi) uliyoyaona na kuyasikia wenyewe (Yesu)
Akimwaga damu yake msalabani tukombolewe
Tuliyoyaona na kuyasikia wenyewe (hivyo)
Maisha yangu na uhai wangu mimi namkabidhi Yesu
Amewaponya wenye magonjwa wakawa huru
Akawafufua wafu nao wakawa hai
Ni nani kama Yesu na hakuna aliye kama Yesu
Alitoa uhai wake kwa ajili yetu
Akafa kifo cha aibu pale msalabani
Ni nani kama Yesu na hakuna aliye kama Yesu
Ametuachia karamu iliyo kuu,
Karamu ya upatanisho nay a upendo
Ni nani kama Yesu na hakuna aliye kama Yesu
Alibadilisha maji yakawa divai
Na wenye harusi wakanywa wakafurahi
Ni nani kama Yesu na hakuna aliye kama Yesu
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.