SectionsExitMbona Nahangaika

Mbona Nahangaika

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,LentExit
Chorus

{ Mbona nahangaika, mkiwa mimi,

Sina hata wa kunifuta machozi } *2

Ni aibu gani iliyonitanda,

Najuta hata siku ya kuzaliwa kwangun{ Maskini mimi, nitakuwa mgeni wa nani,

Nakulilia e Mungu uniokoe } *2

Verse 2

Taabu na matatizo yanisonga mimi

Shida nazo karaha zanisumbua mimi,

Mungu ufanye hima uniokoe.

Verse 3

Nimeugua nikilalama, mnyonge mimi,

Sina rafiki wala mtetezi, mkiwa mimi

Wote wamenigeuka kuniwinda,

Verse 4

Kila waliwazalo juu yangu ni baya,

Kuugua kwangu kumbe ni furaha kwao

Walitaka nife nisahaulike.

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.