SectionsEntranceMfalme Wa Amani

Mfalme Wa Amani

Ordinary Time,EasterEntrance
Verse 1

Mfalme wa amani mpeni heshima,

Yerusalem mjini anaingia

Na unyenyekeo na upole mkuu

Anapanda punda Mwana wa Mungu.

Chorus

Hosana juu, hosana Juu, hosana juu.

Verse 3

Njooni Mahebruni, njooni watoto,

Leteni matawi ya kumsalimu.

Mwana wa Daudi kweli Masiya

Anakuja kwenu mwenye huruma.

Verse 4

Tandikeni nguo miguuni pake,

Imbeni zaburi, shangilieni.

Mbarikiwa huyu ajaye kwetu

Kwa Jina la Bwana Mkombozi mkuu.

Verse 5

Ufurahi sana, we` Yerusalem

Yule wamwabudu roho za mbingu.

Na huruma pale anakujia,

Haki na amani akuletea.

Verse 6

Ndimi za wachanga zafumbulia,

Kwa mwujiza sifa yake Masiya

Na makundi yote ya malaika

Sifa na heshima wanamtolea.

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.