{ Sasa ni wakati mwafaka wa kutoa sadaka yako ndugu
Hima ndugu jitolee kwa moyo wa ukarimu } *2
Iwe ni fedha pia hata mali umtolee Muumba wako
Akulindaye akuamshaye akupaye hewa na afya njeman{ Waumini, wote tuamke pamoja na sasa tujenge kanisa
Kanisa letu litasitawi kwa michango michango yetu } *2
Kwa moyo wako wa ukarimu mpe muumba wako
Sadaka yako kama shukrani yako
Ujiulize kwa jinsi gani, Bwana kakubariki
Umtolee kama shukrani yako.
Wiki hii nzima amekulinda sasa jifikirie
Ni kitu gani kiwe dhamana yako
Umshukuru kwa jinsi gani naye afurahie
Kwa mema mengi anayotenda kwangu,
Wewe mzima ni wengi sana leo hawaamki
Jifikirie ni wangapi umetenga
Na familia yako daima shida haziwakumbi
Si kwamba hao ni bora kuliko wote.
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.