SectionsThanksgivingMilele Milele Msifuni

Milele Milele Msifuni

Easter,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeThanksgiving
Verse 1

Milele milele msifuni Bwana

Na ahimidiwe Bwana milele,

Amina, amina, aleluya

Rehema za Bwana ni za milele

Na uaminifu wa Mungu wetu,

Ni kwa vizazi hata vizazi

Chorus

{ Njooni, tuimbe, tumwimbie Bwana

Yeye (ndiye) wokovu, wokovu wetu (Bwana)

Ni Mungu wetu na mwumba wetu, aleluya aleluya } *2

Verse 3

Nitakushukuru ee Bwana Mungu

Nitalishukuru jina la Bwana,

Ee Bwana mfalme Mungu wangu

Pigeni vigelegele pigeni

Pigeni magoti mbele za Bwana

Kwa maana ndiye Mungu wetu

Verse 4

Atawabariki wamchao Bwana

Wadogo wakubwa awabariki

Msaada wao na ngome yao

Tazama atabarikiwa hivyo

Atabarikiwa amchaye Bwana

Awabariki toka Sayuni

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.