Chorus
[s] Mimi mzabibu wa kweli, mimi mzabibu wa kweli,
Nanyi m matawi yangu, Baba yangu ni mkulima,
Mwenye kutunza shamba lake } *2n[s] Tawi lile lisilozaa
Baba yangu huliondoa, na kuliteketeza moto,n[s] Tawi lile linalozaa
Baba yangu hulisafisha, lidumu katika kuzaa
Hayo - hayo ni maneno ya Bwana Yesu }*2
Verse 2
Nyinyi mmekwisha, kuwa wasafi,
Kwa sababu ya neno, nililowaambia
Kaeni nami, ndani yangu,
Na mimi na mimi na mimi ndani yenu
Verse 3
Akaaye ndani yangu, huyo atazaa
Kwani nje yangu, hataweza kuzaa
Kama vile nje ya mzabibu,
Tawi halitaweza kamwe kuzaa.
Verse 4
Maneno yangu yakikaa ndani mwenu,
Ombeni lolote mtatendewa
Naye Baba yangu atatukuzwa,
Na nyinyi mtakuwa wanafunzi wangu
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.