SectionsEucharistMimi Mzabibu Wa Kweli

Mimi Mzabibu Wa Kweli

Easter,Easter,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeEucharist
Chorus

[s] Mimi mzabibu wa kweli, mimi mzabibu wa kweli,

Nanyi m matawi yangu, Baba yangu ni mkulima,

Mwenye kutunza shamba lake } *2n[s] Tawi lile lisilozaa

Baba yangu huliondoa, na kuliteketeza moto,n[s] Tawi lile linalozaa

Baba yangu hulisafisha, lidumu katika kuzaa

Hayo - hayo ni maneno ya Bwana Yesu }*2

Verse 2

Nyinyi mmekwisha, kuwa wasafi,

Kwa sababu ya neno, nililowaambia

Kaeni nami, ndani yangu,

Na mimi na mimi na mimi ndani yenu

Verse 3

Akaaye ndani yangu, huyo atazaa

Kwani nje yangu, hataweza kuzaa

Kama vile nje ya mzabibu,

Tawi halitaweza kamwe kuzaa.

Verse 4

Maneno yangu yakikaa ndani mwenu,

Ombeni lolote mtatendewa

Naye Baba yangu atatukuzwa,

Na nyinyi mtakuwa wanafunzi wangu

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.