Chorus
{ Mimi ni mtumishi wake Bwana, nitendewe ulivyonena *2
Nitendewe ulivyonena, mimi ni mtumishi wa Bwana } *3
Verse 2
Salamu uliyejaa neema, Bwana yu pamoja nawe
Usiogope Maria, Mungu kakupendelea
Verse 3
Tazama utapata mimba utazaa mwana, utamwita jina Yesu,
Huyu atakuwa mkuu, ataitwa mwana wa aliye juu
Verse 4
Bwana Mungu atampa kiti cha enzi, cha Baba yeke Daudi
Ataitawala nyumba ya Yakobo hata milele
Ufalme wake hautakuwa na mwisho
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.