Verse 1
Utukufu kwa Mungu juu mbinguni,
Na amani iwe kwa watu wenye
Mapenzi mema duniani kote.
Chorus
Tunakusifu,
Tunakusifu, tunakuheshimu, tunakuabudu,ntunakutukuza.
Verse 3
Tunakushukuru, Mungu kwa ajili,
Ya ‘tukufu wako mkuu, ee Bwana, ni
Mungu ndiwe Mfalme wa mbinguni
Verse 4
Ee Baba Mwenyezi, Bwana Yesu Kristu,
Ee Mwana wa pekee, ee Mungu Mwana
Kondoo wa Mungu, Mwana wake Baba.
Verse 5
Mwenye kuondoa dhambi za dunia,
Utuhurumie, ‘tuhurumie,
Maombi yetu, Bwana, uyapokee.
Mwenye kuketi kuume kwa Baba,
Verse 6
Utuhurumie, kwa kuwa ndiwe
Pekee yako ni Mtakatifu
Verse 7
Pekee yako, Bwana, pekee yako mkuu,
Ewe Yesu Kristu, pamoja naye
Roho Mtakatifu milele yote.
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.