Amani ya dunia imetoweka
Tumuombe Mwenyezi aturudishie
Tamaa ubinafsi vilivyoshamiri
Ni sumuyo amani tunayohitaji
{
Aa-eh njooni wote
Aa-eh tusali pamoja
Aa-eh tuombee amani
Hatari inatukabili
Tumuombe Mungu atuepushen} * 2
Mizinga maroketi imetayarishwa
Madege ya kutisha ituangamize
Ngao yetu wanyonge ... ...
Yatubidi tusali vita tutashindan
Ujambazi wa kutisha umetuandama
Mali yathaminiwa kuliko uhai
Twahitaji ulinzi wa Mungu Mwenyezi
Aombaye hupewa, njooni tuombe
Ndani ya familia moto unawaka
Kupigwa tusi mateke sasa ndizo sala
Watoto nao pia ni vurugu tupu
Hawana mchungaji kwenye familia
Wito umetolewa tusali rozari
Baba Mtakatifu anatuhimiza
Matendo ya rozari tuyatafakari
Naye Mama wa Mungu atatusikia
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.