Chorus
{ Moyo wangu unakutamani,
Moyo wangu unakutamani Mungu wangu } *2n{ Kwa sauti nzuri mimi nikuimbie ee Mungu wangu,
Nitangaze sifa zako milele na hata milele } *2
Verse 2
Nikuambie nini Bwana, ujue ninakupenda
Moyo wangu umekuambia uso wako nitautafuta
Usinifiche uso wako ee Mungu Muumba wangu
Verse 3
Umenitendea mambo mengi, makubwa ya kushangaza
Sasa mimi nitazitangaza fadhili zako Bwana wangu
Asubuhi hata usiku ee Mungu nitakusifu
Verse 4
Nibariki ee Mungu wangu, siku zote za maisha yangu
Nikusifu wewe daima nitangaze uwezo wako
Usiwe mbali Mungu wangu naomba usiniache.
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.