SectionsEucharistMoyo Wangu Unakutamani

Moyo Wangu Unakutamani

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeEucharist
Chorus

{ Moyo wangu unakutamani,

Moyo wangu unakutamani Mungu wangu } *2n{ Kwa sauti nzuri mimi nikuimbie ee Mungu wangu,

Nitangaze sifa zako milele na hata milele } *2

Verse 2

Nikuambie nini Bwana, ujue ninakupenda

Moyo wangu umekuambia uso wako nitautafuta

Usinifiche uso wako ee Mungu Muumba wangu

Verse 3

Umenitendea mambo mengi, makubwa ya kushangaza

Sasa mimi nitazitangaza fadhili zako Bwana wangu

Asubuhi hata usiku ee Mungu nitakusifu

Verse 4

Nibariki ee Mungu wangu, siku zote za maisha yangu

Nikusifu wewe daima nitangaze uwezo wako

Usiwe mbali Mungu wangu naomba usiniache.

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.