SectionsThanksgivingMoyo Wangu Wa Utulie

Moyo Wangu Wa Utulie

Lent,Ordinary TimeThanksgiving
Chorus

Moyo wangu na utulie kwako Bwana Mungu wangu - na mwokozi wangu

Maana wewe Bwana ndiwe kimbilio langu - tena mlinzi wangu *2

Chorus

Wewe ndiwe Bwana - wa neema

Fadhili zako - ni za milele

Nikupe nini - Bwana mimi nikushukuru

Umenipa Bwana - na uhai

Pia na nguvu - za kutembea

Nafsi na roho - zangu kweli zimeridhika x2

Verse 3

Asubuhi niamkapo nitalisifu jina lako,

Kwa nyimbo nzuri za furaha mchana mimi nitaimba,

Usiku utimiapo, mimi nitakushukuru,

Kwa maana ninaishi kwa neema zako.

Verse 4

Kila nitembeapo mimi naona utukufu wako,

Wewe waniongoza mimi, kila hatua nipigayo,

Wewe ni Mungu mkuu, na mwenye Baraka tele,

Ninazo sababu tele za kukusifu wewe.

Verse 5

Ewe Bwana unanijua hata ndani ya moyo yangu,

Unaziona siri zangu hata wajua nitakalo,

Ninakuomba ee Bwana, uyajibu maombi yangu,

Kwa kuwa wewe ndiwe tumaini langu

Verse 6

Moyo wangu hukutafuta mchana hata na usiku,

Na mimi ninapokuita kweli wewe huniitika,

Karibu uishi kwangu, nami niwe ndani yako

Usikubali Bwana nitangane na wewe

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.