Mpendane Daima
Mungu akaona si vyema mtu huyu awe peke yake
Nitamfanyia mwenzake yule wanafanana naye
Akaumba mwanamke, kamleta kwake mwanamume waishi pamoja
{ Ewe Bwana - mpokee mke wako tangu leo
Ewe Bibi - mpokee mume wako tangu leo
Muishi nyote pamoja, mpendane daima
Msitengane daima, msivunje agano } *2
Mungu akawapa uwezo watawale viumbe vyote
Mungu akasema zaeni muijaze dunia kwa watu
Baraka za Mungu Baba, zimewashukia tangu leo zaeni matunda
Ewe mwanamume mpende mke wako kwa moyo wote
Nawe mwanamke heshimu mume wako mtii daima,
Ndoa ni maagano, kati ya watu wawili wapendanao
Nyumba yenu iwe hekalu lake Mungu kanisa ndogo
Nyumba ya amani upole na furaha nyumba ya sala
Mungu ameunganisha mwanadamu asitenganishe daima dawamu
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.