SectionsExitMpende Adui

Mpende Adui

Ordinary TimeExit
Verse 1

Bwana Yesu alituachia amri ya mapendo

Ili tupendane kama yeye alivyotupenda

Tena akasema, akasisitiza,

Mpende jirani, kama nafsi yako

Chorus

{ Mpende - adui yako

Mpende - muombee neema

Mpende - adui yako

Mpende - muombee Baraka } *2

Verse 3

Sisi tulivyoumbwa wanadamu hatulingani

Kwa tabia kwa maisha hata kwa matendo yetu

Wapo wa hekima, wasemao ukweli,

Na wenye kiburi, wasio na busara

Verse 4

Hata ukinyanyaswa jitahidi kuvumilia

Usiwe mwenye ghadhabu ukalipiza kisasi

Ukihuzunishwa, mkimbilie Yesu,

Atakupa faraja, heri na fanaka

Verse 5

Usikumbuke ubaya uliokwisha tendewa,

Hiyo itakuwa njia ya kukaribisha chuki

Ukisha samehe, usahau yote,

Ukatae yote, yasiyo ya hekima

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.