Verse 1
Bwana Yesu alituachia amri ya mapendo
Ili tupendane kama yeye alivyotupenda
Tena akasema, akasisitiza,
Mpende jirani, kama nafsi yako
Chorus
{ Mpende - adui yako
Mpende - muombee neema
Mpende - adui yako
Mpende - muombee Baraka } *2
Verse 3
Sisi tulivyoumbwa wanadamu hatulingani
Kwa tabia kwa maisha hata kwa matendo yetu
Wapo wa hekima, wasemao ukweli,
Na wenye kiburi, wasio na busara
Verse 4
Hata ukinyanyaswa jitahidi kuvumilia
Usiwe mwenye ghadhabu ukalipiza kisasi
Ukihuzunishwa, mkimbilie Yesu,
Atakupa faraja, heri na fanaka
Verse 5
Usikumbuke ubaya uliokwisha tendewa,
Hiyo itakuwa njia ya kukaribisha chuki
Ukisha samehe, usahau yote,
Ukatae yote, yasiyo ya hekima
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.