SectionsOffertoryMpeni Kaisari

Mpeni Kaisari

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Wedding,Ordinary Time,Ordinary TimeOffertory
Verse 1

Vipaji tumepewa, mapato tumepata

Lakini binadamu tunashindwa kushukuru

Wakati tunaomba, tunajinyenyekesha

Lakini tukipata mikono yetu birika

Chorus

Mpeni kaisari, yaliyo yake

Mpeni Mungu (yale) yaliyo yake Mungu *2

Verse 3

Mifugo tunafuga, nafaka tunavuna

Lakini kila siku tunakula na kusaza

Kumbuka kuna wale, wasio na chochote

Hawawezi kupata, hata kikombe cha chai

Verse 4

Tunapofanya kazi, twapata mishahara

Shughuli zetu sisi kuingia kwenye baa

Ikiwa zitabaki, twakuja kanisani

Twamtolea Mungu, shilingi moja na tano

Verse 5

Tukiwa na wagonjwa hatuwasaidii

Wakati wamekufa tunachanga kwa huzuni

Twachukua mikopo, kwa mambo ya anasa

Ujenzi wa kanisa, twalazimishwa kutoa.

Verse 6

Kumbuka Ibrahimu, alitoa mwanawe

Kama sadaka kwake Mungu Baba wa mbinguni

Na sisi kwa furaha, tupeleke zawadi

Itakayopendeza, kama ile ya Abeli

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.