SectionsExitMshike Mshike

Mshike Mshike

Ordinary TimeExit
Chorus

{ Hebu wanadamu na tufikirie sasa ni wapi tutakwenda,

Vita vimezidi amani hakuna shetani ametia nanga } *2

Mshike mshike kila kona watu wakimbilia usalama

Lo! Lo! hili jambo limekuwa kawaida

Ona wazee na watoto wateseka

Mshike mshike, mshike mshikenmshikeshike huu utaisha lini?n(Tumuombe Mungu), atikise huu mshikemshike

Verse 2

Ulimwengu wote umekuwa na visa vya ajabu,

Pande moja vita pande nyingine mambo ya ajabu

Tujisitiri wapi, kila pande machungu,

Tunakuomba ee Mwenyezi utupe usalama Baba

Verse 3

Watu nao wamekuwa wakali kuliko wanyama

Tunaishi kama hakuna kizazi kingine tena

Vita vya kila siku, uhasama wa mali,

Kizazi chetu kimekuwa dhiki tena ukiwa sana

Verse 4

Ulimwengu nao umekuwa jeneza la vijana,

Kuvaa vibaya madawa makali wanatumia

Eti wao wajanja, waenda na wakati

Hawajui maisha yana mwisho silaha yao pombe

Verse 5

Hebu fikiria unayefanya mambo haya yote,

Ujue ya kuwa kila lenye mwanzo linao mwisho,

Acha ya kidunia, faida ya ukiwa

Mtegemee Mungu unayo nafasi hii kabla hujafa

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.