SectionsExitMungu Na Shetani

Mungu Na Shetani

Ordinary Time,Ordinary Time,Lent,Ordinary Time,Lent,Ordinary TimeExit
Verse 1

Ndugu yangu sikia nasema kwa makini,

Habari hii kuu ya ufalme wa Mungu

Inasikika sana, sasa imeenea,

Lakini sio wengi, wanaoiamini

Chorus

Waimbaji tumeshaimba nyimbo nyingi

Makasisi wamehubiri pande nyingin{ Twasema uokoke, nawe wasema kesho

Inapofika kesho, wasema kesho kutwa

Siku nazo zapita, miaka inapita

Uchague mwenyewe, Mungu au shetani } *2

Verse 3

Ukizipata shida, walaumulaumu,

Ndugu na majirani, wadhani umelogwa

Unaanza ugomvi, wachukia wengine,

Hata bila sababu wawaita wachawi

Verse 4

Waomba mara moja, ukikosa majibu,

Kesho inapofika waenda kwa mganga

Ngoja nikueleze, Mungu hana haraka,

Jifunze vumilia majibu utapata

Verse 5

Jifikirie ndugu, usingoje ya kesho,

Muda ni wako sasa, amua ukubali

Mengi tumeyasema, ilobaki ni kwako,

Uchague mwenyewe, Mungu au shetani

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.