Mungu Yule

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Lent,Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeThanksgiving
Chorus

{ Nimemuona yule ninayemtafuta na neema zake

Nimemuona -leo nimemuona Mungu } *2n

Mkononi mwake ana uzima tena ni wa milele

Mkononi mwake ana uzima ninaoutafuta

Na uzima huo anatoa bure kwa walio tayari

Lakini kuna kanuni moja ya kwamba, uwajali watu.

Verse 2

Nimemuona Mungu yu mtupu-u hana nguo

Anatamani mimi niende nikamvishe

Nimemuona Mungu ana njaa hana chakula

Anatamani mimi niende nikamlishe

Nimemuona Mungu ni mgonjwa-a kitandani

Anatamani mimi niende kumtazama

Verse 3

Nimemuona Mungu amefungwa-a gerezani

Anatamani mimi niende kumfariji

Nimemuona Mungu ni mkimbizi mpakani

Anatamani mimi niende kumpokea

Nimemuona Mungu ni yatima hana wazazi

Anatamani mimi niende nikamtunze

Verse 4

Nimemuona Mungu ni mjane hana matunzo

Anatamani mimi niende kumhifadhi

Nimemuona Mungu amefiwa ana majonzi

Anatamani mimi niende kumfariji

Nimemuona Mungu ni kilema na hajiwezi

Anatamani mimi niende kumuinua

Verse 5

Nimemuona Mungu atolewa angali mimba

Anatamani mimi niende kumtetea

Nimemuona Mungu anapigwa kwa makombora

Anatamani mimi niende kusuluhisha

Nimemuona Mungu ni mtumwa ananyanyaswa

Anatamani mimi niende kumtetea

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.