SectionsExitMvivu Wewe

Mvivu Wewe

Ordinary TimeExit
Chorus

Mvivu wewe mvivu * 3 mvivu wewe

Hebu watazame wadudu hawa

Hebu watazame sisimizi wewe

Wana adili ya kazi pasipo kusimamiwan(Tazama wanavyojituma (jituma) hawalazimishwi

Tena hawana kiongozi (yeyote) wa kuwapangia)*2n{Ewe mvivu utalala we! we! hatarini

Utaondoka lini katika usingizi wako? }*2

Verse 2

Kwa wenzako kunapokucha, wewe nd'o unalala

Wenzako wanapoamka, wewe wajigeuza

Wenzako wakipanga majukumu, wewe waota ndoto

Wenzako wanapotoka kazini, wewe watupa shuka

Verse 3

Wenzako wanafanya kazi, tena kwa kujituma

Wenzako wanafanya kazi, tena kwa moyo mmoja

Daima wewe wajivuta, tena wingi wa maneno

Hata nazo salamu haziishi, tena sababu mia mia.

Verse 4

Hebu jitazame sasa, umbeya wakutawala,

Tena ukijichunguza, na wizi wakuandama

Wenzako wakifanikiwa, waanza kazi kuwaomba,

Na maisha ya jirani, wewe wayafuatilia

Verse 5

Jiulize utabarikiwa, lini ewe mvivu,

Jiulize utaamka, lini ewe mvivu,

Ukishiba leo huwazi, ya kesho utakula nini

Hakuna lolote ufanyalo bila ya kusimamiwa.

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.