SectionsEntranceMwamba Wenye Imara

Mwamba Wenye Imara

Ordinary Time,LentEntrance
Verse 1

Mwamba wenye imara, kwako nitajificha

Maji hayo na damu, yaliyo toka humu

Hunisafi na dhambi, hunifanya mshindi

Verse 2

Kwa kazi zote pia, sitimizi sheria

Nijapofanya bidii, nikilia na kuudhi

Hayaishi makosa, niwe wa kuokoa

Verse 3

Sina cha mkononi, naja msalabani

Nilitupu, nifike, ni mnyonge, nishike

Nilimchafu naja, nioshe nisijafa

Verse 4

Nikungojapo chini, na kwenda kaburini,

Nipaapo mbinguni, na kukwona enzini

Roho yangu naiwe, rahani mwako wewe

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.