SectionsEntranceMwimbieni Bwana Zaburi

Mwimbieni Bwana Zaburi

Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeEntrance
Chorus

Mwimbieni Bwana zaburi

Mwimbieni kwa kinubi) *2n{Mwimbieni kwa kinubi na sauti ya zaburi

Mwimbieni kwa panda na sauti ya baragumu (wote)

Shangilieni mbele za mfalme Bwana wa majeshi}

Verse 2

Bahari na ivume na vyote viijazavyo,

Ulimwengu na wote wanaokaa ndani yake

Milima naiimbe kwa furaha mbele za Bwana Mungu

Verse 3

Wanyama wa mwituni na mimea ya kondeni

Upepo na uvume kupeleka habari hizi

Kwa ndege wa angani na viumbe vilivyo baharini

Verse 4

Nikitazama kushoto kulia nyuma na mbele

Nikitazama angani nikitazama ardhini

Kila nionacho kinasimulia utukufu wako

Verse 5

Kwa maana mbingu na dunia ni kazi yako

Jua na mwezi na nyota anga pia nayo mawingu

Ni kazi ya vidole vyako na ujuzi wa mikono yako

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.