Chorus
Mwimbieni Bwana zaburi
Mwimbieni kwa kinubi) *2n{Mwimbieni kwa kinubi na sauti ya zaburi
Mwimbieni kwa panda na sauti ya baragumu (wote)
Shangilieni mbele za mfalme Bwana wa majeshi}
Verse 2
Bahari na ivume na vyote viijazavyo,
Ulimwengu na wote wanaokaa ndani yake
Milima naiimbe kwa furaha mbele za Bwana Mungu
Verse 3
Wanyama wa mwituni na mimea ya kondeni
Upepo na uvume kupeleka habari hizi
Kwa ndege wa angani na viumbe vilivyo baharini
Verse 4
Nikitazama kushoto kulia nyuma na mbele
Nikitazama angani nikitazama ardhini
Kila nionacho kinasimulia utukufu wako
Verse 5
Kwa maana mbingu na dunia ni kazi yako
Jua na mwezi na nyota anga pia nayo mawingu
Ni kazi ya vidole vyako na ujuzi wa mikono yako
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.