SectionsOffertoryNakuja Na Zawadi

Nakuja Na Zawadi

Baptism,MarianOffertory
Verse 1

Naondoka mimi naenda kwa Baba,

Nipeleke hiki nilichokipata,

Japo kidogo, sitaona haya,

Nimeamua, sitarudi nyuma

Chorus

{ Nakuja polepole Baba,

Nakuja na zawadi yangu

Naleta mbele zako ili nitoe shukurani } *2

Verse 3

Natembea mimi mwendo wa madaha,

Nakanyaga chini kwa maringo tele,

Naelekea, altare ya Bwana,

Nimkabidhi, nilichojaliwa.

Verse 4

Nimechangamka ninashangilia,

Napiga kelele kelele za shangwe

Nachezacheza, najongea kwako,

Ee Mungu Baba Nipokee mimi.

Verse 5

Nafsi yangu mimi naileta kwako,

Mkate divai pia ninaleta

Uigeuze, mwili na damuyo,

Chakula chetu, tunaosafiri

Verse 6

Mavuno shambani mimi nimevuna,

Mifukoni fedha nimekabidhiwa,

Mimi ni nani, nisikushukuru,

Baba nasema asante kwa yote.

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.