SectionsEucharistNakula Mwili Wa Yesu

Nakula Mwili Wa Yesu

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeEucharist
Verse 1

Nakula mwili wa Yesu, nakunywa damu ya Yesu

Naburudika daima, narukaruka na Yesu

Naimba wimbo wa Yesu, nachezacheza na Yesu

Natembea naye Yesu, naenda kwetu Mbinguni

Chorus

{ Mimi nashangalia, (mimi) mimi naburudika

Yesu ameniponya, kweli nina uzima } *2

Verse 3

Mwalimu wangu ni Yesu, tabibu wangu ni Yesu

Mlinzi wangu ni Yesu, mimi nina usalama

Uhai wangu ni Yesu, mapito yangu ni Yesu,

Naenda na Bwana Yesu, naelekea Mbinguni

Verse 4

Rafiki wangu ni Yesu, jabali wangu ni Yesu

Mshindi wangu ni Yesu, mimi nitashinda vita.

Mpaji wangu ni Yesu , mlishi wangu ni Yesu

Mjali wangu ni Yesu, sina budi kumsifu

Verse 5

Kaeni ndani ya Yesu, kaeni pamoja naye

Na Yesu akae kwenu, mtashinda majaribu

Shikeni maneno yake, jifunzeni kwake Yesu

Yesu atawachukua, awapeleke Mbinguni

Verse 6

Maisha ya duniani, pasipo Yesu ni bure

Uzima wa ulimwengu, bila Yesu ni hapana

Kuleni mwili wa Yesu, kunyweni damu ya Yesu

Onjeni damu ya Mbingu, mtaishi siku zote

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.