Chorus
Napiga goti langu (Bwana), nainamisha kichwa (chini)n{Kukuomba ewe Mungu-, unifungue moyo-
Nipate kushiriki- karamu takatifu-
Ili roho yangu dhaifu ipate wokovu} * 2
Verse 2
Furaha ya moyo wangu ni wewe Bwana
Matumaini ya moyo wangu ni kwako
Ninajongea sasa kushiriki karamu takatifu, Bwana, wangu
Verse 3
Ninaitikia mwaliko wako Bwana
Moyo wangu unatetemeka kwa hofu
Mwaliko wako umejaa upendo kwangu moyoni
Verse 4
Kila tuulapo mwili wa Bwana Yesu
Na kuinywa damu tunapata uzima
Tumekombolewa kwa damu yake Mwanakondoo, Mwana wake Mungu
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.