SectionsEntranceNi Siku Kubwa

Ni Siku Kubwa

Wedding,Ordinary Time,Ordinary Time,WeddingEntrance
Verse 1

Ni siku kubwa njooni nyote tushangilieni

Kweli kwa shangwe na tupigeni vigelegele

Twaomba Mungu Baba Awabariki awajalie na watoto

Verse 2

Ni siku kuu ya harusi siku ya furaha

Kwani wawili wamepatana kufunga ndoa

Lindeni ndoa yenu Ili kwa dhiki wala faraja msitengane

Verse 3

Mungu alipomuumba mwanamume Adamu

Akamuumbia mwanamke waishi pamoja

Agano lake Mungu Msilivumje, msilitupe, mhifadhi.

Verse 4

Basi wewe mwanamume umpende mke wako

Umlinde na kumtunza asiwe na upweke

Umlinde siku zote Hadi mwenyezi Mungu atakapoamua

Verse 5

Na wewe mwanamke umpende mume wako tu

Na watoto mtakaojaliwa naye Mungu

Uwatunze kwa wema, na kanisani uwapeleke kwake Mungu

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.