SectionsEucharistNinakuabudu Mungu Wangu

Ninakuabudu Mungu Wangu

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeEucharist
Verse 1

Ninakuabudu Mungu wangu,

Unayejificha altareni,

Ninakutolea moyo wangu,

Usiofahamu siri yako.

Verse 2

Mafahamu yangu yadanganya,

Yanapokuona na kugusa,

Namsadiki Yesu hadanganyi,

Yeye Mungu Mwana na ukweli

Verse 3

Waficha Umungu msalabani,

Na ubinadamu altareni,

Nami naungama zote mbili,

Kama mwivi yule mwenye toba.

Verse 4

Thomas aligusa majeraha,

Nami nasadiki bila shaka

Ewe Yesu nipe pendo lako,

Tumaini kwako na imani

Verse 5

Umeteswa nini Bwana mwema,

Kwa kunipa mkate wa uzima

Yesu unifiche ndani yako,

Ili nilionje pendo lako

Verse 6

Yesu Pelikane nitazame,

Na kwa damu yako nitakase

Tone moja ndilo linatosha,

Na dunia yote yaokoka

Verse 7

Ndani ya mafumbo Yesu yumo,

Atafunguliwa kwangu lini?

Nikuone Yesu uso wako,

Nishiriki nawe heri yako. Amina.

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.