Ninakuabudu Mungu wangu,
Unayejificha altareni,
Ninakutolea moyo wangu,
Usiofahamu siri yako.
Mafahamu yangu yadanganya,
Yanapokuona na kugusa,
Namsadiki Yesu hadanganyi,
Yeye Mungu Mwana na ukweli
Waficha Umungu msalabani,
Na ubinadamu altareni,
Nami naungama zote mbili,
Kama mwivi yule mwenye toba.
Thomas aligusa majeraha,
Nami nasadiki bila shaka
Ewe Yesu nipe pendo lako,
Tumaini kwako na imani
Umeteswa nini Bwana mwema,
Kwa kunipa mkate wa uzima
Yesu unifiche ndani yako,
Ili nilionje pendo lako
Yesu Pelikane nitazame,
Na kwa damu yako nitakase
Tone moja ndilo linatosha,
Na dunia yote yaokoka
Ndani ya mafumbo Yesu yumo,
Atafunguliwa kwangu lini?
Nikuone Yesu uso wako,
Nishiriki nawe heri yako. Amina.
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.