SectionsEntranceNjooni Tumwimbie

Njooni Tumwimbie

Pentecostal,Ordinary Time,Wedding,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeEntrance
Chorus

Njooni tumwimbie Bwana wetu - kwa shangwe

Njooni kwa masifu kwa nderemo - tuchezen{Njooni tuabudu, njooni tusujudu

Tupige makofi,

Mbele zake Bwana, Mungu wa ulimwengu } *2

Verse 2

Hekalu lake Bwana Mungu linapendeza,

Nyumbani mwake Bwana mna mengi mazuri

Ninatamani kuingia nyumbani mwake

Nikae naye siku zote nyuani mwake

Nipate heri, mbele za Bwana

Verse 3

Mapema leo ninabisha lango ee Bwana

Nifungulie nipokee nipe faraja

Nimelemewa na mizigo mingi ya dhambi

Nyumbani mwake Bwana ndiko kuna uzima

Uzima tele, na usalama

Verse 4

Twendeni sote kwake Bwana Mungu Mwenyezi

Twendeni kwake tupeleke maombi yetu

Tutoe shukrani zetu kwa Mungu Baba

Tutoe na dhabihu zetu kwake Muumba

Sadaka zetu, azipokee

Verse 5

Uhai wetu unatoka kwake Muumba

Tuimbe sifa zake Mungu siku kwa siku

Tuyatangaze maajabu yake popote

Tuseme Bwana ametenda mambo makuu

Kwa watu wote, milele yote.

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.