Chorus
(Nyanyukeni waumini wote tufanye shangwe
Kwa nderemo, kwa vigelegele na kwa vifijo ) *2
Bwana asifiwe (sana) Bwana asifiwe (kweli)
Bwana asifiwe Mwathani aragoshuo
Verse 2
Nikiziangalia mbingu ni kazi ya vidole vyake,
Mwezi na nyota za mbinguni ulizoratibisha wewe.
Verse 3
Uwezo wake Bwana Mungu haupimiki kwa mizani,
Mipango yake kwetu sisi haiwezi kubadilishwa.
Verse 4
Alikausha baharí ya Shamu ikawa nchi kavu,
Waisraeli wakapita kwa uwezo wa Mungu Baba.
Verse 5
Na tupigeni tarumbeta vinubi hata na matari,
Tuimbe wimbo wake Musa na ule wa Mwanakondoo.
Verse 6
Pazeni sauti zenu kwa shangwe hata na vifijo,
Sifa pia na utukufu tumpe Bwana siku zote.
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.