SectionsEntranceNyanyukeni Waumini

Nyanyukeni Waumini

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeEntrance
Chorus

{ Nyanyukeni waumini wote tufanye shangwe

Kwa nderemo, kwa vigelegele na kwa vifijo } *2

Bwana asifiwe (sana) Bwana asifiwe (kweli)

Bwana asifiwe Mwathani aragoshuo

Verse 2

Nikiziangalia mbingu ni kazi ya vidole vyake

Mwezi na nyota za mbinguni ulizoratibisha wewe

Verse 3

Uwezo wake Bwana Mungu haupimiki kwa mizani

Mipango yake kwetu sisi haiwezi kubadilishwa

Verse 4

Alikausha baharí ya Shamu ikawa nchi kavu

Waisraeli wakapita kwa uwezo wa Mungu Baba

Verse 5

Na tupigeni tarumbeta vinubi hata na matari

Tuimbe wimbo wake Musa na ule wa Mwanakondoo

Verse 6

Pazeni sauti zenu kwa shangwe hata na vifijo

Sifa pia na utukufu tumpe Bwana siku zote

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.