Chorus
{ Nyanyukeni waumini wote tufanye shangwe
Kwa nderemo, kwa vigelegele na kwa vifijo } *2
Bwana asifiwe (sana) Bwana asifiwe (kweli)
Bwana asifiwe Mwathani aragoshuo
Verse 2
Nikiziangalia mbingu ni kazi ya vidole vyake
Mwezi na nyota za mbinguni ulizoratibisha wewe
Verse 3
Uwezo wake Bwana Mungu haupimiki kwa mizani
Mipango yake kwetu sisi haiwezi kubadilishwa
Verse 4
Alikausha baharí ya Shamu ikawa nchi kavu
Waisraeli wakapita kwa uwezo wa Mungu Baba
Verse 5
Na tupigeni tarumbeta vinubi hata na matari
Tuimbe wimbo wake Musa na ule wa Mwanakondoo
Verse 6
Pazeni sauti zenu kwa shangwe hata na vifijo
Sifa pia na utukufu tumpe Bwana siku zote
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.