Verse 1
Mama yetu Maria, ni mama wa neema, tena ni kimbilio la watu wote wakosefu, ni msaada wa kweli mama tuombee
Chorus
Ni Nyota, ni Nyota, mama yetu Maria ni Nyota ya matumaini x2
Verse 3
Mlango wa mbinguni, sanduku la agano, malkia wa amani, malkia mwenye huruma, mama mpendelevu mama tuombee
Verse 4
Nyota ya asubuhi, ni mnara wa pembe, kimbilio la wakosefu mama utuombee, mama yetu Maria kiongozi wetu
Verse 5
Twakushukuru mama kwa maombezi yako, na kwa neema zote unazo tuombea mama, malkia wa amani mama tuombee
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.